RAIS SAMIA AKUTANA NA RAIS WA INDONESIA IKULU DAR ES SALAAM

Rais Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Joko Widodo, wakati alipowasili katika Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam kuanza ziara ya kikazi hapa nchini.


Rais Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Joko Widodo, wakati Wimbo wa Taifa wa Tanzania na Indonesia ukiimbwa katika Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais Widodo amewasili nchini kwa ziara ya kikazi.


Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Joko Widodo, akikagua gwaride la heshima baada ya kuwasili katika Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ziara ya Kikazi hapa nchini.


Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza na Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Joko Widodo, wakati alipowasili katika Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam kuanza ziara ya kikazi hapa nchini. (Picha zote na Ikulu).



Powered by Blogger.