FIRST LADY MNANGAGWA AWASILI JIJINI ARUSHA

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Dkt. Auxillia Mnangagwa amewasili jijini Arusha na kupokelewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dkt. Pindi Chana, Naibu Waziri, Dunstan Kitandula, baadhi ya watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii na Sekretarieti ya Shirika la Utalii Duniani.

Mnangagwa anatarajiwa kushiriki Jukwaa la Pili la Kimataifa la Utalii Wa Vyakula la Shirika la Utalii Duniani (UN Tourism) Kanda ya Afrika Aprili 23, 2025 jijini humo.



Powered by Blogger.